Search This Blog

Sunday, November 4, 2012

January Makamba afanya majaribio mfumo wa kuripoti Rushwa



Muda mfupi baada ya kukaririwa na gazeti la the Guardian la nchini Uingereza akiahidi kuanzisha mfumo utakaosaidia wananchi wa Tanzania kuripoti rushwa kwa njia ya simu na mtandao wa internet, jana Makamba amefanya majaribio ya mfumo huo mbele ya wataalam mbalimbali wa social media.

Akitambulisha mfumo huo kwa wadau, January Makamba alisema "Ni asilimia 6.9% ya vitendo vyote vya rushwa nchini ndio vinavyo ripotiwa kwa vyombo husika. Kwahiyo zaidi ya 93% ya matukio ya rushwa hayafikishwi polisi au TAKUKURU. Kutokuwa na ufahamu ya wapi rushwa inatendeka na saa ngapi, ni kizingiti kikubwa katika vita dhidi ya rushwa. Ni matumaini yangu kwamba mRushwa itatoa taarifa kuhusu rushwa ilivyo nchini ili tuweze kuitokomeza".

No comments:

Post a Comment