Search This Blog

Monday, November 26, 2012

Breaking news: Sharo milionea afariki dunia kwa ajali ya gari

Msanii nyota wa vichekesho na uimbaji Sharomillionea (Ramadhan Hussein) amekufa kwenye ajali iliyotokea huko Tanga. Kijana nyota yake ilikua inaanza kung'ara na kupata dili za matangazo akiwa na Mzee Majuto.
Kamanda wa Polisi Tanga akisema “leo majira ya saa mbili usiku kwenye barabara ya Segera Muheza mtu mmoja alietambulika kwa jina la Hussein Ramadhani au Sharo Milionea akiwa anaendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es salaam kwenda Muheza alipofika eneo la Maguzonizonga wilayani Muheza hilo gari lake liliacha njia na kupinduka mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”

Kamanda amesema hakuna kona kali sana wala ubovu wa barabara kwenye sehemu aliyopata ajali Sharo Milionea, katikati ya Segera na Muheza ambapo gari imehifadhiwa mahali salama kwa sababu haitembei.

No comments:

Post a Comment