Search This Blog

Sunday, July 14, 2013

CHADEMA YASHINDA KATA ZOTE NNE UCHAGUZI MADIWANI ARUSHA

Chama cha Demokarasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeibuka Mshindi katika uchaguzi mdogo wa Udiwani uliokuwa ukizihusisha kata za Themi, Kimandolu, Kaloleni pamoja na Elerai ushindi ambao umeonyesha wakazi wa Arusha kuwa na imani kubwa na chama hicho.

Matokeo hayo yamepokelewa kwa furaha kubwa sana na wafuasi wa chama hicho, viongozi pamoja na wafuatiliaji wa masuala ya siasa na wapenda mabadiliko kwa ujumla huku wakisema ushindi huo ni ishara ya wananchi kupaza sauti kwa chama kikongwe cha CCM kuwa wamechoshwa na mambo yalivyo kwa sasa.

Maskikitiko upande wa CCM
1. Kata ya Themi
Chadema= 678
CCM =326
CUF =313

2.Kata ya Kimandolu
Chadema=2665
CCM =1169

3. Kata ya Kaloleni
Chadema =1019
CCM =389
COF =169

4.Kata ya Elerai
Chadema=1715
CCM=1239
CUF =213


Kauli ya Nape kabla ya Matokeo:
Katika majira ya 1:40 alasiri katika hali inayoonyesha Nape Nnauye kutambua matokeo mapema aliandika katika Mtandao wa Kijanii wa Jamiiforums akionyesha kukubali kushindwa mapema. 

Aliandika haya: "Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa)". 

No comments:

Post a Comment