Search This Blog

Wednesday, January 2, 2013

Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga apumzika Tanzania kwa siku saba


Waziri wa Ujenzi John Magufuli wakiagana na Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga





Raila Odinga akiwa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere na mwenyeji wake Magufuli.

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Kenya Raila Odinga amerejea Jijini Nairobi Nchini Kenya baada ya kuwepo nchini Tanzania kwa mapumziko ya siku saba.


Odinga alitumia muda wa mapumziko yake hapa nchini kutembelea maeneo mbali mbali ya kihistoria, mbuga za wanayama na visiwa vya Zanzibar ambako alisherehekea mwaka mpya.


Katika ziara hiyo binafsi, Raila Odinga aliambatana na Mkewe Mama Ida Odinga pamoja na wanafamilia wa karibu. Wakati akiondoka katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, na alielezea kufurahishwa kwake na namna alivyoweza kupokewa na kupata muda mzuri wa mapumziko na kwamba sasa yuko imara kabisa kuendelea na majukumu yake ya kisiasa.
Chanzo: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/378302-raila-odinga-arejea-kenya-baada-ya-mapumziko-mafupi-nchini-tanzania-pichani-akiwa-na-magufuli.html


‘Nimepumzika vizuri na kusherehekea vyema mwaka mpya wa 2013 katika visiwa vya Zanzibar, ninawashukuru wote walioshirikiana na familia yangu na ninawatakia Heri ya Mwaka Mpya’ alimalizia Waziri Mkuu huyo wakati akiagana na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwepo uwanja wa ndege kumsindikiza.

No comments:

Post a Comment