Search This Blog

Monday, January 7, 2013

BREAKING NEWS: ASKARI POLISI WAWILI WAUAWA KARAGWE KWENYE DILI LA MENO TA TEMBO



ASKARI Polisi wawili wa kituo Kidogo cha Polisi Benacco wilayani Ngara mkoani Kagera wameuawa na wananchi baada ya kushambuliwa kwa silaha za jadi huku gari walilokuwa nalo likichomwa moto katika kijiji cha Rugu Chanyamisa wilayani Karagwe mkoani Kagera.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Said Mwema
Askari hao ambao wametambulika kuwa ni Sanjenti Thomas na Koplo Damas wa kituo kidogo cha Polisi Benacco wilayani Ngara, Inasemekana wakiwa na gari aina ya Noha namba hazijatambulika kutokana na gari hilo kuchomwa moto na kuteketea wakiwa na wafanyabishara wawili waliotambulikwa kwa majina ta Shabani Abubakari pamoja na Gerald wote wa Benacco walikwenda huku wafanyabishara hao wakijidai kuwa wanunuzi na baada ya kuonyeshwa shehena ya mzigo huo wa meno ya Tembo waliwabonyeza askari waliokwenda nao na kisha kuyafunga kwenye gunia na wakawageuka wale vijana wauzaji aliyetambulika kwa jina la Raymond na mwenzake mmoja ambao walifanikiwa kukimbia lakini baadaye wakagundua kuwa walichezewa Dili na askari hao hivyo nao kuamua kuwapigia simu wananchi wakiwaeleza kuwa wameibiwa na majambazi huku wakiwatajia aina ya gari na rangi yake.



Alisema baada ya askari hao kuanza kuondoka kurudi benacco wakiwa na Meno ya tembo kufika eneo hilo walikuta njia ikiwa imefungwa kwa mawe na huku kukiwa na kundi kubwa la wananchi wenye siraha za asili na ndipo askari hao waliouawa walipojitokeza na kujitambulisha kwa wananchi lakini walishambuliwa na kuuawa hapo hapo.




Hili ni tukio la pili askari kuuawa na wananchi ambapo katika tukio la kwanza lililotokea Desemba 15 mwaka jana askari wengine wawili  Koplo Pascal na Konstebo Alex wa Kikosi cha Usalama Barabarani wilayani Ngara waliauawa kwa kushambuliwa na wananchi wakati ambapo walikuwa wamekwenda katika kijiji cha Mugoma kwa lengo la kukagua pikipiki mbovu na zisizokuwa na usajili.

Baada ya kupata habari hizo askari hao waliondoka watatu wakiwa na wafanyabishara hao wawili ambao walipokaribia wilayani Karagwe walitangulizwa nyumbani kwa mfanyabiashara huyo ili kuzungumza naye wakijifanya wakitaka kununua meno hayo na baada ya kuonyeshwa waliwapigia simu polisi na kuja kukamatwa.



No comments:

Post a Comment