Search This Blog

Wednesday, August 7, 2013

MFANYABIASHARA WA MADINI JIJINI ARUSHA AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI

Pichani juu askari wakikagua mwili wa  Erasto Msuya, mmoja wa Wafanyabiasha wakubwa wa Madini jijini Arusha aliyejulikana ambaye pia ni mmiliki wa SG HOTEL mkoani humo, baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi na kufa papo hapo.

Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa mfanya biashara huyo alifariki dunia mara baada ya majibishano ya risasi baina ya majambazi hayo na mfanya biashara huyo ambapo alizidiwa  nguvu na kupigwa risasi na kufariki dunia.

Habari zinaeleza na kubainisha zaidi kuwa Marehemu alikuwa akitokea KIA kwenda BOMA ambako alikuwa ameitwa na watu (ambao hawakujulikana mara moja) ili wakafanye biashara.

Uchunguzi unaendelea ikiwa ni pamoja na kujua chanzo cha mauaji yake.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amen.

No comments:

Post a Comment